Dawa Ya Misoprostol

00:01
Misoprostol ni dawa iliyo kundi la prostaglandin. Hujulikana kwa majina kama miso, cytotec. Hutumika katika matibabu ya vidonda vya tumbo, ujauzito na wakati wa kujifungua. Inatumika sana katika utoaji mimba usio salama na wakati mwingine kuleta madhara kama kutokwa damu nyingi na maambukizi kwenye mji wa uzazi.

Namna Inavyofanya kazi

Misoprostol ni aina ya prostagndin ya kutengenezwa ambayo huzuia kuzalishwa kwa tindikali ya tumboni na kusaidia kulinda kuta za tumbo. Kwenye tumbo la uzazi hufanya kuta za uzazi kusinyaa na hivyo mimba kutoka kama mtu alikuwa mjamzito, au damu kutoka kama alikuwa amejifungua.

Matumizi

Hupatikana  katika vidonge vya mikrogramu 100 na 200 (100 and 200 microgram). Vidonge hivi unaweza kunywa, kuweka chini ya ulimi au ndani ya uke ikitegemea na tatizo linalotibiwa. Dawa hii hutumika katika;

  • Kutibu vidonda vya tumbo kutokana na dawa za NSAID.
  • Kutoa mimba.
  • Kuanzisha uchungu wakati wa kujifungua
  • Kuzuia kupoteza damu nyingi baada ya kujifungua

Usalama Wakati Wa Ujauzito

Misoprostol sio salama kabisa kutumika wakati wa ujauzito. Inaharibu mimba.

Tahadhari

Usitumie dawa hii kama una mimba. Inaweza kuharibu ujauzito wako.
Usitumi dawa hii na dawa zenye magneziamu (magnesium) kama antacids.
Kama unatarajia kuwa na ujauzito, mwelezee daktari wako kabla ya kuanza kutumia dawa hii.
Usiache dawa bila kushauriana na daktari wako.
Usinywe pombe wakati unatumia dawa hii.

Madhara

Matumizi ya misoproatol yanaweza kuleta madhara yafuatayo kwa mtumiaji.

  • Kuharisha
  • Tumbo kuuma
  • Kichwa kuuma
  • Kichefuchefu
  • Tumbo kujaa gesi
  • Kutapika
  • Mabadiliko katika hedhi
  • Kupasuka mji wa uzazi

Wahi hospitali kama unatokwa na damu ukeni baada ya kunywa dawa hii.

Kunywa dawa pamoja na chakula ili kuondoa uwezekano wa kuharisha.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »