Elimu

Magonjwa

uzazi

Recent Posts

Vidokezo Muhimu Kukusaidia Kupata Ujauzito kwa Haraka

Vidokezo Muhimu Kukusaidia Kupata Ujauzito kwa Haraka

13:07 Add Comment

 Vidokezo muhimu kukusaidia kupata ujauzito kwa haraka

Unajaribu kupata ujauzito? Mabadiliko rahisi ya maisha ya kila siku yanaweza kukusaidia kuongeza nafasi ya kupata ujauzito. Tazama vidokezo hivi muhimu:


Hatua ya kwanza: Acha sigara

Uvutaji wa sigara unajulikana kupunguza nafasi ya kupata ujauzito kwa wanawake na wanaume. Ni hatari pia kwa mtoto kama bado unavuta sigara na una ujauzito.


Hatua ya pili: Fanya mazoezi pamoja

Kuwa imara kimwili ni njia kubwa ya kuongeza nafasi ya kupata ujauzito. Kama hujazoea kufanya mazoezi, anza sasa. Kwa mfano, unaweza kushuka kituo kimoja kabla ya nyumbani ili upate kutembea zaidi au kutumia ngazi badala ya lifti. Unaweza kujiunga na darasa la kucheza au kukimbia mchakamchaka pamoja.


Hatua ya tatu: Kula chakula chenye afya

Chakula na uzazi vinahusiana. Chakula cha pamoja chenye mlo kamili, kinaweza kuongeza nafasi ya kupata ujauzito. Jaribu pia kutafuta ni vyakula vipi vizuri kwa wanaume na wanawake wanapojaribu kutafuta mtoto.


Hatua ya nne: Pumzika!

Kujaribu kupata ujauzito kunaweza kuchosha. Kwa bahati mbaya, kuwa na mawazo sana inaweza kufanya ugumu kupata ujauzito, hivyo jaribuni kuchukulia mambo kiurahisi. Jipatieni mda wa kupumzika kwa kufanya masaji, mazoezi ya kupumua kwa kina au kufurahia milo ya usiku pamoja. Chochote kinachoweza kuwafanya mpumzike na kuwa katika hali ya utulivu.


Hatua ya tano: Acha pombe

Pombe inaweza mdhuru mtoto kama unakunywa sana baada ya kupata ujauzito,hasa wiki za kwanza kabla ya kugundua una ujazito. Kunywa kwa kupitiliza kunaweza kupunguza nafasi ya kumpa mwanmke ujauzito kwa wanaume. Hivyo, ni vyema wewe na mwenzi wako kuepuka pombe, au kupunguza kabisa, mara mnapopanga kutafuta mtoto.


Hatua ya sita: Mwanaume kuepuka korodani kuwa katika hali ya joto sana.

Wakati korodani zikipata joto sana, mbegu za kiume zinateseka. Kukaa mda mrefu kutumia laptop kwenye mapaja, au kufanya kazi katika mazingira yenye joto inaweza kuleta madhara katika utengenezaji wa mbegu za kiume. Inashauriwa, kuepuka kuvaa nguo za ndani (boxer) zenye kubana, ingawa hakuna ushahidi mwingi kwa hili. Ikiwa una matumaini ya kuwa baba ni wakati mzuri wa kuacha kutumia laptop kwa kuweka kwenye mapaja na kuvaa nguo zenye kukupa uhuru.



Hatua ya saba: Chukua likizo pamoja

Mapumziko au wikiendi ndefu pamoja inaweza kuwasaidia kupunguza msongo wa mawazo, na kufurahia mapumziko pamoja. Kiukweli, baadhi ya wazazi wameapa mapumziko ya pamoja yenye nia ya kutafuta mtoto (conceptionmoon) ni njia kuu ya kupata mimba.


Hatua ya nane: Fufua nuru katika mapenzi

Kama imeshindikana kuenda mapumziko,au kupata likizo, jaribu njia nyingine za kufufua mapenzi. Baadhi ya wanandoa wengi wanahisi wanafanya mapenzi kujaribu kupata ujauzito. Kama hili ni jambo linalokukumba, jaribu kurudisha mwanga katika mapenzi yenu.


Hatua ya tisa: Fanya mapenzi (kujamiana) mara kwa mara
Kujamiana ni muhimu sana! Hata kama unaja lini yai litapevushwa, kufanya mapenzi mara mbili hata tatu itakupa nafasi nzuri ya kupata ujauzito.


Matumizi Ya Dawa Wakati Wa Ujauzito

12:19 Add Comment
Ujauzito ni kipindi muhimu sana katika maendeleo na ukuaji wa mtoto tumboni mwa mama. Maendeleo na ukuaji huu unaweza kuathiriwa na vitu mbalimbali ikiwemo baadhi ya dawa zinazotumika wakati wa ujauzito.

Mjamzito anapokunywa dawa, dawa hunyonywa na kuingia kwenye damu ambapo huweza kuingia kwa mtoto kupitia kondo la uzazi. Baadhi ya dawa zinaweza kuleta madhara kwa mtoto tumboni ambayo yataathiri ukuaji wake. Kwa hiyo ni muhimu sana kuwa mwangalifu na dawa unazotumia wakati wa ujauzito. Ikumbukwe si dawa zote zitaathiri ukuaji wa mtoto.

Usalama Wa Dawa

Dawa hufanyiwa uchunguzi wa usalama wake wakati wa ujauzito. Utafiti huu huanza kufanyika kwa wanyama. Tafiti za kiepidemiolojia zinaweza kufanyika kuthibitisha usalama kwa binadamu wakati wa ujauzito. Hizi hufanyika kwa kutazama dawa wajawazito walizotumia na kama kuna madhara yaliyotokea kwa mtoto.

Pia usalama wa dawa hutofautiana kulingana na ukubwa wa mimba, kuna dawa ambazo si salama wakati wa miezi 3 ya kwanza lakini huweza kutumika miezi 4 na kuendelea ya mimba.

Mamlaka ya Dawa na Chakula Marekani (Foods and Drugs Authority – FDA) inagawanya dawa katika makundi 5 kutokana na usalama wake wakati wa ujauzito. Makundi haya ni:

  • Kundi A – Dawa hizi ni salama kutumia wakati wa ujauzito. Hazina madhara kwa mtoto tumboni wakati wa ujauzito na wakati wa kunyonyesha.
  • Kundi B – Salama kuitumia. Hakuna athari zinazoonekana kwa binadamu ingawa zinaweza kuwepo kwa wanyama wengine.
  • Kundi C – Zinaweza kuwa na madhara kwa mtoto. Tafiti kwa wanyama zinaonesha dawa hizi zinaweza kumdhuru mtoto tumboni, au hakuna ushahidi wa kutosha. Zinatumika pale ambapo faida ni muhimu ili kuokoa maisha ya mjamzito.
  • Kundi D – Kuna ushahidi wa madhara kwa mtoto tumboni. Itumike kuokoa maisha pale ambapo maisha ya mama yapo hatarini na hakuna dawa nyingine mbadala isipokuwa hiyo.
  • Kundi X – Hairuhusiwi kabisa kutumika wakati wa ujauzito.
Baadhi ya dawa ambazo ni salama wakati wa ujauzito ni Amoxicillin, Ampicillin, Clindamycin, Erythromycin, Penicillin na Nitrofurantoin.

Baadhi ya dawa zilizothibitishwa kuwa tishio kwa afya ya mtoto wakati wa ujauzito ni Streptomycin, Tetracycline, Cyclophosphamide, Cocaine, Methotrexate, Kanamycin, Ethanol, Valproic acid na Phenobarbital.

Madhara ya Dawa Wakati Wa Ujauzito kwa Mtoto

Dawa nyingi huleta madhara hasa miezi 3 ya mwanzo wa ujauzito. Hiki ni kipindi ambacho viungo mbalimbali vya mtoto huanza kutengenezwa, hivyo dawa pamoja na kemikali mbalimbali huweza kuathiri uumbaji wa viungo hivi na kuleta matatizo. Baadhi ya madhara yatokanayo na matumizi holela ya dawa wakati wa ujauzito ni:

Kupata maumbile yasiyo kawaida (malformations) ambayo yanaweza kuathiri kichwa, ubongo, moyo, figo, miguu,mikono na viungo vingine vya mwili.
Kutokua vizuri
Kufariki akiwa tumboni
Mtoto kudumaa tumboni
Mtoto kuzaliwa na uzito mdogo sana, njiti.
Mtoto kuzaliwa kabla ya wakati (premature birth)
Mimba kuharibika
Utindio wa ubongo

Mambo Ya Kuzingatia Kuhusu Dawa

Tumia dawa pale ambapo ni muhimu sana kutumika na ugonjwa umethibitishwa.
Mueleze daktari wako kuwa una ujauzito. Ni muhimu ajue ili usipewe dawa ambazo zinaweza kuwa na madhara kwa mtoto wako.
Kama unatarajia kuwa mjamzito, kuwa makini na matumizi ya dawa hasa wiki 2 baada ya kupata siku za hedhi kwani mimba inaweza kuwa imetunga lakini dalili hazijaanza bado.
Kama una tatizo au ugonjwa unaohitaji kunywa dawa kila siku, mueleze daktari wako palo unapofikiria kupata ujauzito.
Ni muhimu kuwa makini na matumizi ya dawa na kemikali mbalimbali sio tu wakati wa ujauzito bali hata kabla ya ujauzito na kipindi chote unachotarajia kuwa na mimba.
Kama italazimu kutumia dawa wakati wa ujauzito, basi hakikisha na daktari wako kuwa dawa ni salama na haitaleta madhara kwa mtoto tumboni mwako.

Maumivu Wakati Wa Kukojoa

10:12 Add Comment
Maumivu wakati wa kukojaoa ni hali inayotokea kwa watu wengi ikisababishwa na magonjwa mbalimbali. Maumivu wakati wa kukojoa hujulikana kwa kitaalamu kama dysuria. Kati ya sababu kuu zinazosababisha maumivu wakati wa kukojoa ni maambukizi ya mfumo wa mkojo (Urinary tract Infection – UTI) hasa kwa wanawake na magonjwa ya zinaa

Maumivu Wakati wa Kukojoa Yanavyotokea 

Maumivu wakati wa kukojoa hutokana na kuchubuka kwa njia ya mkojo. Kuchubuka huku hutokea pale njia ya mkojo inaposhambuliwa na bakteria au kemikali na kuharibu ukuta wa juu wa njia ya mkojo hivyo huwa kama kidonda. Pale mkojo unapopita eneo hili basi unapata maumivu kama ya kuungua. Maumivu haya yanaweza kutokea wakati wote unakojoa, mwanzoni au mwishoni mwa kukojoa.

Kwa watoto wadogo, mara nyingi hulia wakati wanakojoa ikiwa wanapata maumivu kwani hawawezi kuongea.

Pia yanaweza kuambatana na dalili nyingine kama homa, kutokwa na usaha au uchafu sehemu za siri, kutokwa mkojo wenye damu damu, maumivu chini ya kitovu au maumivu ya ubavu (flanks).

Sababu za Maumivu Haya

Maumivu haya hutegemea na chanzo cha ugonjwa unaoleta dalili hii. Baadhi ya vyanzo vya maumivu wakati wa kukojoa ni:

Maambukizi ya njia ya mkojo (UTI)

Ugonjwa huu huleta maumivu kama ya kuungua kwenye njia ya mokojo. Pia maumivu yanaweza kufika mpaka chini ya kitovu wakati wa kukojoa. Dalili nyingine zinazoweza kuambatana na hali hii ni homa, kukojoa mara kwa mara, kuhisi mkojo hauishi kwenye kibofu na maumivu ya mgongo.

Magonjwa ya zinaa

Magonjwa ya zinaa kama kisonono na klamidia huleta maumivu wakati wa kukojoa hasa kwa wanaume, maumivu haya huwa kama ya kuungua wakati mkojo unatoka. Dalili nyingine zinazoweza kuambatana na magonjwa haya ni kutoa uchafu kama usaha sehemu za siri, maumivu chini ya kitovu na homa.

Kichocho

Kichocho husababisha maumivu wakati wa kukojoa ikiambatana na kutoa mkojo wenye damu.

Magonjwa mengine yanayoweza kusababisha maumivu wakati wa kukojoa ni:
  • Mawe ya Figo (kidney stones)
  • Maambukizi ya ukeni (vaginitis)
  •  Saratani ya kibofu cha mkojo
  •  Kuchubuka kwa njia ya mkojo kutokana na ajali, kupigwa, kuendesha farasi au mazoezi mengine.
  •  Kuwekewa mpira wa mkojo (urinary catheter) au kuingizwa vipimo vya njia ya mkojo au kibofu (instrumentation of urethra or bladder).

vipimo

Vipimo vifuatavyo vinaweza kufanyika ili kujua chanzo cha maumivu wakati wa kukojoa.

  •  Kipimo cha uchunguzi wa mkojo (urinalysis)
  •  Kuotesha mkojo (urine culture)

Uchunguzi za mkojo na kuotesha mkojo huweza kuonesha kama kuna maambukizi kwenye njia ya mkojo. Pia mabaki ya mawe ya figo huweza kuonekana.

  •     Kipimo cha Ultrasound ya tumbo na kiuno (Pelvic and abdominal ultrasound).
Kipimo hiki huweza kuonesha matatizo ya kwenye figo ikiwemo mawe ya figo, uvimbe kwenye mfumo ya mkojo au maambukizi ya figo. Vipimo vingine kama X-ray au CT Scan vinaweza kufanyika kama dalili nyingine zikiashiria hivyo.

Matibabu

Maumivu wakati wa kukojoa ni dalili, hivyo matibabau huelekezwa kwa ugonjwa unaoleta tatizo hili. Maumivu haya yanaweza kutibiwa na kupona kabisa. Ikiwa mtu atapata tena maambukizi yaliyoleta dalili hii awali, basi maumivu haya yanaweza kujirudia tena.

Wahi kwenye kituo cha kutoa huduma za afya uonapo dalili kama hii haraka. Endapo dalili nyingine zinatokea kama damu kwenye mkojo, homa au maumivu ya kwenye ubavu usipoteze muda

Dawa Ya Misoprostol

00:01 Add Comment
Misoprostol ni dawa iliyo kundi la prostaglandin. Hujulikana kwa majina kama miso, cytotec. Hutumika katika matibabu ya vidonda vya tumbo, ujauzito na wakati wa kujifungua. Inatumika sana katika utoaji mimba usio salama na wakati mwingine kuleta madhara kama kutokwa damu nyingi na maambukizi kwenye mji wa uzazi.

Namna Inavyofanya kazi

Misoprostol ni aina ya prostagndin ya kutengenezwa ambayo huzuia kuzalishwa kwa tindikali ya tumboni na kusaidia kulinda kuta za tumbo. Kwenye tumbo la uzazi hufanya kuta za uzazi kusinyaa na hivyo mimba kutoka kama mtu alikuwa mjamzito, au damu kutoka kama alikuwa amejifungua.

Matumizi

Hupatikana  katika vidonge vya mikrogramu 100 na 200 (100 and 200 microgram). Vidonge hivi unaweza kunywa, kuweka chini ya ulimi au ndani ya uke ikitegemea na tatizo linalotibiwa. Dawa hii hutumika katika;

  • Kutibu vidonda vya tumbo kutokana na dawa za NSAID.
  • Kutoa mimba.
  • Kuanzisha uchungu wakati wa kujifungua
  • Kuzuia kupoteza damu nyingi baada ya kujifungua

Usalama Wakati Wa Ujauzito

Misoprostol sio salama kabisa kutumika wakati wa ujauzito. Inaharibu mimba.

Tahadhari

Usitumie dawa hii kama una mimba. Inaweza kuharibu ujauzito wako.
Usitumi dawa hii na dawa zenye magneziamu (magnesium) kama antacids.
Kama unatarajia kuwa na ujauzito, mwelezee daktari wako kabla ya kuanza kutumia dawa hii.
Usiache dawa bila kushauriana na daktari wako.
Usinywe pombe wakati unatumia dawa hii.

Madhara

Matumizi ya misoproatol yanaweza kuleta madhara yafuatayo kwa mtumiaji.

  • Kuharisha
  • Tumbo kuuma
  • Kichwa kuuma
  • Kichefuchefu
  • Tumbo kujaa gesi
  • Kutapika
  • Mabadiliko katika hedhi
  • Kupasuka mji wa uzazi

Wahi hospitali kama unatokwa na damu ukeni baada ya kunywa dawa hii.

Kunywa dawa pamoja na chakula ili kuondoa uwezekano wa kuharisha.

Vyakula Vinavyofaa Kwa Mjamzito

23:13 Add Comment

Lishe bora wakati wa ujauzito ni muhimu sana, kwani lishe hii hutumika kwa mama na mtoto anaendelea kukua tumboni. Kwa kawaida mahitaji ya chakula na virutubisho mwilini mwa mwanamke huongezeka wakati wa ujauzito na kadri ujauzito unavyoendelea kukua, virutubisho hivyo hutumika kujenga mwili wa mama na mtoto. Hivyo maamuzi ya lishe au lishe mama anayopata huathiri pia maendeleo ya mtoto anayekua mwilini mwake. Tutaona vyakula muhimu vya kuzingatia lishe bora wakati wa ujauzito na baadhi ya vitu vya kukwepa. Mlo kamili (balanced diet), ni muhimu kwa ajili ya maendeleo mazuri ya afya ya mjamzito na mtoto tumboni. Pamoja na mlo kamili mjamzito hupewa virutubisho ziada (supplements) kwa ajili ya kuongeza madini kama ya chuma na Foliki. Mlo kamili unajumuisha vyakula vya wanga, protini, mafuta, vitamini, madini na maji kama inavyochambuliwa hapa chini

Nafaka na Vyakula vya Wanga.

Vyakula hivi huupa mwili nguvu za kufanya kazi ikiwemo ukuaji wa mtoto tumboni. Vyanzo vya wanga ni kama nafaka mbalimbali(mahindi,mtama,ulezi n.k), viazi, ndizi, mihogo. Ni vizuri mjamzito awe anapata nafaka kamili(whole grains) kama mahindi, ngano na mchele usiokobolewa; cereals n.k.

Nyama, Samaki na Vyakula vya Protini.

Hivi ni muhimu kwenye kuujenga mwili, hasa kipindi cha miwezi wa 4 mpaka wa 9 ambacho viungo mbalimbali vya mtoto vinajengwa. Ni muhimu mama apate vyakula vya protini vya kutosha ili kuhakikisha ukuaji wa mtoto unaenda vizuri. Nyama za kuku, ng’ombe, mbuzi, senene, panzi na wanyama wengine ; vyanzo vya protini za mimea kama maharage, soya, njugu, njegere, karanga,korosho n.k . Samaki, maziwa, mayai ni vyanzo vingine vya protini muhimu.

Vyakula vya Mafuta.

Hutumika kwenye kuupatia mwili nguvu pamoja na ujengaji wa seli za mwili. Mara nyingi vyakula kama nyama, karanga, ufuta, alizeti,senene, panzi, samaki na matunnda kama maparachichi huwa na mafuta. Ni vizuri kutumia mafuta yatokanayo na mimea ili kupunguza mafuta yenye lehemu(cholesterol) nyingi.

Mboga za Majani na Matunda.

Matunda na mboga za majani ni sehemu muhimu sana ya mlo wakati wa ujauzito, kwani huupatia mwili vitamini, madini na kambakamba kwa ajili ya kulainisha chakula. Vitamini husaidia kuimarisha kinga ya mwili sambamba na ufanyaji kazi wa mwili.  Madini kama ya chuma, kalsiamu, zinki, madini joto(Iodine) na magneziamu ni muhimu kwa ukuaji salama wa mtoto tumboni mwa mama.

Vitamini B9 (Foliki asidi) na madini ya chuma hutolewa kama virutubisho ziada kliniki wakati wa ujauzito ili kutosheleza mahitaji ya mwili na kuzuia hatari ya upungufu wa damu kutokea.

Maji

Maji ni muhimu kwenye mmenyenyo na unyonywaji wa chakula, pia husaidia kuzuia choo kigumu, mwili kuvimba na maambukizi ya mfumo wa mkojo (UTI). Inashauriwa mjamzito anywe maji si chini ya lita 2.3 kwa siku, yanaweza kuwa katika chai, juisi, soda, au maji yenyewe. Ni vema zaidi kama akinywa maji kama maji zaidi na kupunguza vinywaji kama soda.

Mfano wa Mpangilio wa Mlo.

Ili kuhakikisha mlo kamili mjamzito anaweza kufuata mfano wa mpangilio wa mlo ufuatao;

Mfano,
Mlo wa Asubuhi:    A – Chungwa/ Embe/ Ndizi mbivu/ Parachichi,  B – Mkate/ Maandazi/ Chapati/ Vitumbua,Uji      C – Karoti    D – Mayai,    E – Maziwa/ Mtindi/ Siagi/ Maziwa ya  Soya
Mlo wa Mchana:     A – Parachichi/ Papai/ Ndizi/ Embe na chungwa,  B – Ugali/ Wali/ Ndizi/ Makande/ Tambi          C – Mchicha/ matembele/ Mnavu/ Kisamvu/ Spinach/ Kabeji,      D – Maharage/ Samaki/ Kuku/ Njugu/ Nyama/ Dagaa        E – Maziwa/ Mtindi/ Siagi/ Maziwa ya  Soya.
Mlo wa Usiku:        A – Parachichi/ Papai/ Ndizi/ Embe na Chungwa,   B – Wali/ Ndizi/ Viazi/ Tambi/ Chapati          C – Mchicha/ Matembele/ Mnavu/ Kisamvu/ Spinach/ Kabeji,      D – Maharage/ Samaki/ Kuku/ Njugu/ Nyama/ Dagaa           E – Maziwa/Mtindi/Siagi/Maziwa ya  Soya.

Vitu na Vyakula vya kuepuka/kupunguza

Matumizi ya Pombe wakati wa ujauzito huathiri mtoto. Haishauriwi kutumia pombe kabisa!
Uvutaji Sigara
Kupunguza unywaji wa kahawa au vinywaji vyenye caffeine nyingi.
Samaki aina ya papa, swordfish, tilefish na king mackerel kwani wana mekuryi kwa wingi amabayo ni mbaya kwa afya.

Dalili Za Ujauzito

14:07 Add Comment
Mwanamke anapopata ujauzito, mwili wake hupata mabadiliko yanayotokana na homoni mbalimbali zinazobadilika pale yai lake linaporutubishwa na mbegu za kiume. Mabadiliko haya huleta dalili mbalimbali ambazo huashiria ujauzito. Ingawa sio lazima mwanamke apate dalili hizi zote ili kuashiria ujauzito, anaweza akapata chache kati ya hizi;

  • Kukosa Hedhi 
 Hii ni dalili ya mwanzo ya ujauzito.  Kukosa hedhi kwa zaidi ya siku 10 toka siku ambayo mtu alikuwa anategemea kupata hedhi yake,  huashiria kuwa ni mjamzito. Kukosa hedhi mwezi unaofuta huongeza zaidi uwezekano wa kuwa mjamzito.  Ikumbukwe pia kukosa hedhi kunaweza kusababishwa na vitu vingine ukiacha ujauzito.

Baadhi ya wanawake wanaweza wakapata damu kidogo (vaginal spotting) kwa siku moja au mbili katika kipindi wanachotegemea hedhi. Hii inatokana na mimba kuwa inapandikizwa kwenye tumbo la uzazi. Damu huwa kidogo na hedhi huwa ya muda mfupi ukilinganisha na hedhi ya kawaida.

  • Kichefu chefu na Kutapika
Hali ya kichefuchefu na kutapika hasa wakati wa asubuhi hujitokeza mwanzoni mwa ujauzito mpaka miezi mitatu au minne ya ujauzito. Hii huambatana na kukosa hamu ya kula baadhi ya vyakula. Kadri ujauzito unavyokua na hii hali hupungua. Huwapata zaidi ya theluthi mbili za wanawake wenye ujauzito. Kwa baadhi ya wanawake inaweza kuendelea wakati wote wa ujauzito.

  • Kizunguzungu na Kichwa kuuma
 Hali ya kizunguzungu hutokea kwa baadhi ya wanawake, hasa mwanzoni mwa ujauzito na kisha huaacha kadri mimba inavyoendelea kukua. Wakati mwingine inaweza kuambatana na kichwa kuuma. Mara nyingi ni hali ya mpito, na hivyo huacha baada ya muda.

  • Kukojoa Mara kwa mara
 Miezi ya mwanzo ya ujauzito huleta hali ya kukojoa mara kwa mara, na kuhisi mkojo hauishi. Hii inatokana na tumbo la uzazi kukandamiza kibofu cha mkojo wakati mimba inakua.

  • Mwili Kuchoka
 Hali ya mwili kuchoka hutokea sana mwanzoni mwa ujauzito, mara nyingi inatokana na mabadilikoya homoni ambayo mwili unaanza kuyapata kutokana na ujauzito.

  • Maziwa Kujaa na Kuuma
 Baadhi ya wajawazito hupata mabadiliko katika maziwa, yakiwemo kujaa na kuuma pale yanapoguswa.  Mabadiliko ya kihomoni husababisha hali hii kutokea.

  •  Kununa au kukasirika ghafla na mara kwa mara (mood swings). 
Kuna wajawazito hupata hii hali. Ni rahisi kukasirika ghafla na wakati mwingine kununa au kutojisikia furaha. Baadhi hufikia mpaka kiwango cha kuwanunia wenzi wao. Kwa hiyo hapo uvumilivu unahitajika kwa kweli!

  • Tumbo kuwa kubwa 
 Kadri muda unavyoenda, tumbo la mimba huwa linakuwa na kuanza kuonekana mara nyingi kuanzia miezi 3 ya ujauzito.

  • Kuthibitisha Ujauzito 
 Dalili tulizoona mara nyingi huashiria ujauzito, lakini sio uthibitisho wa ujauzito. Hivyo ni muhimu kwenda hospitali uthibitishe kwa vipimo kwani kuna magonjwa ya mfumo wa uzazi yanayoweza kuleta dalili kama hizo. Vipimo vifuatavyo hufanyika kuthibitisha ujauzito:

  • Kipimo cha Ujauzito cha Mkojo (Urinary Pregnancy Test).
 Unaweza ukafanya kipimo hiki hospitali au mwenyewe ukinunua kwenye duka la dawa.  Kipimo hiki kinaweza  kupima ujauzito kuanzia wiki 2 toka mara ya mwisho kufanya mapenzi. Hupima homoni ya Human chorionic gonadotropin kwenye mkojo.  

  •  Kipimo cha Ultrasound.

Ultrasound hufanyika kuthibitisha ujauzito, kama upo kwenye tumbo la uzazi na umri wa ujauzito. Kipimo hiki hufanyika hospitali.

Baada ya kuthibitisha ujauzito;
  • Panga kituo cha afya  na siku ya kuanza kliniki ya wajawazito ndani ya miezi 3 ya kwanza. Ukienda na mwenzi wako.
  • Zingatia mlo kamili wakati wa ujauzito, soma hapa zaidi.
  • Epuka kabisa unywaji wa pombe. Pata dondoo zaidi za afya wakati wa ujauzito hapa.


 Meningitis; uvimbe wa utandu wa ubongo na uti mgongo ni nini?

22:45 Add Comment

 

Huu ni ugonjwa unaothiri sehemu inayofunika ubongo na uti wa mgongo, yaani utandu. Ubongo unafunikwa na sehemu au tandu tatu nyembamba za seli ili kuitengenisha na fugu la kichwa. Tandu hizi zinaweza kuathirika na kusababisha hali inayojulikana kama uvimbe wa utandu wa ubongo na uti wa mgongo.

Kwa sababu tandu zilizoathirika ziko karibu na ubongo, uvimbe wa utandu wa ubongo huwa na athari kwenye ubongo na hata kazi zake kama vile kuona, kusikia, kukumbuka, uwezo wa kutembea, uwezo wa kuzungumza na uwezo wa kukumbuka.

NI NINI HUSABABISHA UGONJWA HUU?
Aghalabu husababishwa na bacteria, lakini pia huweza kusababishwa na viumbehai kama virusi na fungi Bakteria hii hupumuliwa ndani na hupenya kupitia damu na kuathiri ubongo na uti wa mgongo. Huambukiza haraka sana/husambaa haraka sana katika maeneo ambapo kuna msongamano mkubwa na hii inaweza kugeuka kuwa mlipuko wa magonjwa.

MLIPUKO NI NINI?
Mlipuko ni ugonjwa unaoambukiza haraka na huathiri watu wengi kwa wakati mfupi sana. Mlipuko, aghalabu hutokea katika sehemu/maeneo makubwa ambapo huishi kariby sana hususan karibu na kambi za wanajeshi, kambi za wakimbizi, katika shule za bweni na kadhalika. Milipuko ya magonjwa hutokea mara moja moja miongoni mwa jamii mbalimbali/tofauti tofauti kwa wakati tufauti tofauti kwa mwaka.
NI NANI ALIYE KATIKA HATARI YA KUPATA UGONJWA HUU?
Kila mtu hupo katika hali ya hatari kuambuwa na kuugua wakati wa mlipuko/mkurupuko huu. Huambuza kirahisi na harka kutoka kwa mtu mmoja hadi mwengine.
Ilivyo kwenye magonjwa yote, ugonjwa wa utandu wa ubongo huathiri sana watoto walio chini ya miaka 5 pamoja na wakongwe. Wale walio na kinga duni k.v wale wanougua ugonjwa wa sukari, saratani, ukimwi, pia wapo katika hali ya kupata ugonjwa wa utandu wa ubongo na uti wa mgongo.

NITAJIZUIA VIPI ILI NISIPATE UGONJWA HUU?
Uzuiaji nzuri ni kupitia chanjo. Lazima watoto wote wachanjwe ili kupunguza hatari ya kuugua ugonjwa wa utandu wa ubongo.
Hata wakati wa mkurupuko wakati mwingine kuna chanjo ya kizuia maambuzi ya ugonjwa huu.
Kwa sababu ugonjwa huu huambukiza kutoka na kukaribiana kwa watu, ni muhimu kuzingatia usafi na kuwa mbali na waathiriwa wa ugonjwa wakati wa kuwatazama, kuwajulia hali ama kuwaliwaza.
Msongamano wa watu ndicho chanzo muhimu cha kuenea na kusambaa kwa ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja hadi mwengine. Katika kupunguza msongamano karibu na wewe, pia unahitajika kupunguza uwezo wa kuzuia magonjwa mengine mbali na utandu wa ubongo.
NITATAMBUAJE NINAPOUGUA UGONJWA HUU? (DALILI NA ISHARA)
Ugonjwa huu huwa na joto la hali ya juu, shida ya kuona au kuepuka mwangaza, basi ni bora uende kwenye hospitali iliyo karibu nawe haraka iwezekanavyo. Hii ni muhim sana panapokuwa na mlipuko wa utandu wa ubongo na utu wa ubongo. Hii ni kwa sababu ugonjwa huu huambuza kwa kasi sana.
Usikawie ni vema kuwa na afya badala ya kujuta.

JE, KUNA TIBA YA UGONJWA HUU?
Ndiyo: huu ni ugonjwa unaosababishwa na bacteria na kuna dawa za kupambana na magonjwa yababishwayo na hewa katika hospitali zote, ambayo yanaweza kutiba ugonjwa wa utandu wa ubongo kabisa. Dawa hizi hutumiwa kupitia sindano mara nyingi kwa siku na lazima sindano hizi ziendelee kwa kipindi cha wiki/majuma mawili hadi matatu.
Iwapo kuna kukawia kufika hospitalini, dawa hiyo haiwezi kusaidia kutibu mgonjwa ambaye amezidiwa na ugonjwa huu. Haitafanya kazi kwa vyovyote vile. Kwa hivyo ni muhimu kuenda hospitalini kwa wakati unaofaa dalili zinapoonekana.
KUTAKUWA NA UBAYA GANI IWAPO SIPATI MSAADA? (MATATIZO)
Ugonjwa wa utandu wa ubongo huambukiza haraka na kwa sababu ni hatari, husabisha kifo iwapo hautibiwi. Wagonjwa wote wa utandu wa ubongo lazima walazwe hospitalini kwa sababu huzingatiwa kuwa dharura ya kimatibabu. Aghalabu, hili hujiri mgonjwa anapoenda hospitalini akichelewa ili kupata matibabu.
Madhara hufungamana na utendakazi wa ukongo na huhusisha upofu, usiwi na kutoweza kutumia mikono na miguu vizuri, kutozungumza kwa ufasaha and nafuu siyo nzuri.

NITAMTUNZA VIPI MTU AMBAYE ANAUGUA UGONJWA HUU (UTANZAJI WA NYUMBANI)?
Haushauriwi kumtunzia mgonjwa wa utandu wa ubongo nyumbani. Hii ni dharura ya kimatibabu inayostahili kutatuliwa hospitalini kati ya wiki 2-3. Iwapo unashuku kwamba Fulani wanaugua ugonjwa huu, wapeleke hospitalini haraka iwezekanavyo.
Wanapokuwa kwenya matibabu na sasa wamerudi nyumbani, husalia kuwa wanyonge. Kwa Hivyo vema kwao kutunzwa. Sharti chakula chao kiwe chepesi chenye na virutubishi wape kiasi kidogo kila baada ya saa mbili. Hii ni kwa sababu hamu yao ya chakula imerudi chini. Watie moyo wagonjwa ambao wana madhara kutokana na ugonjwa huu.
HOJA MUHIMU KUHUSU UGONJWA WA UTANDU WA UBONGO
·         Utandu ni ugonjwa wa ubongo na uti wa mgongo unaotibika. Husambaa haraka sana katika maeneo palipona msongamano na iwapo hautatibiwa.
·         Huathiri sana sana watoto an wakongwe lakini wakati wa mlipuko/mkumpuko huathiri vijana wanaume na wanawake wape watoto kinga kupitia chanjo.
·         Dalili za ugonjwa wa utandu, joto la hali ya juu, kutapika, kuumwa kichwa na kuepuka mwangaza. Kupitia kwa shingo huwa dalili ya mwisho. Watoto walio chini ya miaka 2 wanaweza kuwa na joto tu pamoja na kulia.
·         Ugonjwa wa utandu unaweza kuua kati ya saa au siku chache. Iwapo unaushuku, mkimbize mtoto au mtu mzima hospitalini kwa ajili ya kupimwa. Wanaweza kulazwa kwa ajili ya matibabu.